Waliosema kabla hujafa hujaumbika wala hawakukosea, kwa sababu wapo watu wengi tunawafahamu walikuwa wazima lakini sasa hawana baadhi ya viungo, huku wengine wakiwa kitandani hawawezi kufanya kitu chochote. Leo hii mfahamu mwanaume mmoja kutoka nchini Marekani anayefahamika kwa jila la Paul Alexander, wenye umri wa miaka 77 amevunja record ya kuishi zaidi miaka 70 kwenye pafu la chuma. Paul aliugua Polio akiwa na umri wa miaka 6 mwaka 1952 ambao ugonjwa huo ulimpelekea kupooza na mapafu yake kuharibika hivyo hulazimaki kutumia kifaa cha chuma kwaajili ya upumuaji (Iron Lung). Licha ya wengi kutokuwa na imani kama ataishi muda mrefu, lakini Paul hakukata tamaa ndipo mwaka 2020 aliandika kitabu, kilichoelezea maisha yake kwenye mapafu ya chuma, haikuwa rahisi kwani alitumia miaka mitano hadi kukamilisha kitabu hicho, na kila neno aliliandika yeye mwenyewe bila kutegemea usaidizi wa mtu. Kifaa alichotumia kuandikia kitabu hicho ni kalamu iliyounganishwa kwenye fimbo, na alitumia mdo...